Deuteronomy 31:1-6

Yoshua Kutawala Baada Ya Musa

(Hesabu 27:12-23)

1Kisha Musa akaenda akasema maneno haya kwa Waisraeli wote: 2 a“Sasa nina miaka mia moja na ishirini nami siwezi tena kuwaongoza. Bwana ameniambia, ‘Hutavuka Yordani.’ 3 b Bwana Mwenyezi Mungu wenu, yeye mwenyewe atavuka mbele yenu. Ataangamiza mataifa haya mbele yenu, nanyi mtaimiliki nchi yao. Pia Yoshua atavuka mbele yenu, kama Bwana alivyosema. 4 cNaye Bwana atawafanyia watu hao kile alichowafanyia Sihoni na Ogu, wafalme wa Waamori, ambao aliwaangamiza pamoja na nchi yao. 5 d Bwana atawakabidhi kwenu, nanyi lazima mwatendee yale yote niliyowaamuru. 6 eKuweni imara na moyo wa ushujaa. Msiogope wala msifadhaike kwa sababu yao, kwa kuwa Bwana Mwenyezi Mungu wenu anakwenda pamoja nanyi; kamwe hatawaacha wala hatawatupa ninyi.”

Copyright information for SwhKC